Familia ya wakarmeli imeundwa na watu mbalimbali ambao wanavutwa na maisha ya kiroho ya wakarmeli. Kundi la kwanza ni la mafrateri (Friars). Yaani mapadre na wasio mapadre. wamonaki wa kiume, wamonaki wakaa pweke -waeremiti (hermits), Masista wa maisha ya ndani yaani wamonaki (Nuns), masista wa maisha ya kitume na walei wanaopokea Skapulari ya karmeli. Kila kundi huishi maisha ya namna yake. Lakini wote hawa wanaunganishwa na utamaduni wa maisha ya kiroho ya wakarmeli.