Naitwa GABRIEL JOHN MTITI mzaliwa wa jimbo katoliki la BUNDA parokia ya Mtakatifu Paulo BUNDA . Nilizaliwa tarehe 12/11/1997 nikiwa mtoto watatu kati ya watoto wanne ,wavulana tukiwa watatu na msichana mmoja .
Nilianza elimu ya msingi mwaka 2004 hadi 2010 katika shule ya msingi iitwayo Miembeni B na baada ya hapo nilichaguliwa kwenda kuendelea na masomo ya secondary katika shule ya serikali iitwayo Dr Nchimbi secondary lakini wazazi waliamua kunipeleka Rombo na kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2011 hadi 2014 katika shule ya Shauritanga secondary school inayo ongozwa na jumuiya ya wazazi ya chama cha mapinduzi CCM . Baada ya kumaliza kidato cha nne nilichaguliwa na serikali kujiunga na kidato cha tano huko Wilaya Ludewa mkoa wa Njombe katika shule iitwayo Chief kidulile secondary kwa mchepuo wa Chemia ,Biologia,Geografia[CBG] kuanzia mwezi wa saba 2015 hadi mwezi wa tano 2017 .Baada ya kumaliza kidato cha sita nilisubirili matokeo namnamo mwezi wa saba matokeo ya kidato cha sita yalikua yametoka nikiwa nimefauru kwa kiwango cha Division two baada ya hapo nilikuja kujiunga na shirika la Bikira Maria wa mlima Karmeli.
Wito wa upadre na utawa ni njia ya kipekee ya kuufikia ukamilifu wa kristo kwa kujifunga hadharani na kuyaishi mashauri ya injili ambayo ni Utii,Ufukara, na Usafi wa moyo. Sauti ya kumtumikia Mungu nilianza kuisikia nikiwa mdogo kipindi nikiwa mtumikizi kuanzia 2006 hadi 2011 katika Parokia ya mtakatifu Paul iliyoko Bunda sababu kubwa zaidi iliyo nifanya mpaka nivutiwe na wito wa upadri na utawa nilivyo kuwa mtumikizi katika parokia yetu kulikua na vigango kumi na nane{18} na wahudumu ambao ni mapadri walikua wawili washirika la Mitume wa Yesu Pd Crisogone Njau Mrina{AJ} na Pd Laurent Kawishe{AJ} ambao walikua wanahudumia vigango hivyo na watu walio kuwa wanahudumiwa walikua ni wengi ukilinganisha na idadi ya mapadri waliopo baada ya kuona hivyo nilipenda na mimi pia kuja kuhudumia taifa la Mungu katika kanisa . Sababu ya pili siku moja usiku2008 nikiwa nimelala niliota nikiwa na hudumia watu wengi kanisani na hiyo ndoto ilikua inajirudia mara kwa mara ndipo nilipo mweleza Paroko wangu Fr Crisogone nakunieleza labda badae unaweza kuwa padri akaniambia pia nisali sana ili niweze kufahamu wito wangu vizuri .Na mnamo mwaka 2013 nilifanikiwa kufamiana na sister paschalina ambaye ni mkarimeli anaye fanya utume wake katika parokia ya Bunda ndipo nilipo mueleza nia yangu ya wito akanimbia natakiwa nikazane katika masomo na kusali sana ili nitambuwe wito wangu vizuri nachague shirika au jimbo nitakalo jiunga nalo baada ya hapo mnamo 2014 mwezi wa kumi na mbili nilikutana na Paschal Dominic {ambaye ni mseminari katika shirika la Bikira Maria wamlima karmeli}katika parokia ya Bunda niliongea nae na kumwomba maelezo ya shirika alilopo alifaniwa kunieleza karama za shirika vizuri mpaka nikavutiwa nazo baada ya hapo nilianza kulifatilia shirika la Bikira Maria wa mlima Karmeli katika website ya shirika ili nipate maelezo ya kutosha zaidi .Nilifanikiwa kupata mawasiliano ya Fr Victor {O.CARM} mnamo Desemba 2016 na kumueleza wito wangu namshukuru Mungu Fr Victor alikua tayari kunisikiliza na kunipokea kwa ajili ya kujiunga na shirika Mnamo 5/07/2017 nilifika nyumba ya malezi ya shirika la Bikira Maria kwa ajili ya kuanza malezi nashukuru nilipokelewa vizuri na nafurahia maisha ya wito huu,zaidi namuomba Mungu aendele kunilinda na kuendeleza yale aliyoanzisha kwangu.
BIKIRA MARIA MAMA YETU WA MLIMA KARMELI
UTUOMBE