KUPATWA KWA JUA SIKU YA JUMA PILI 03 NOV, 2013

KUPATWA KWA JUA SIKU YA JUMA PILI 03 NOV, 2013

Inaanza - 10:24 Jioni

Kati (70%) - 11:28 Jioni

Mwisho - Jua linapochwa, magharibi

Tarehe 3 novemba mwaka huu, siku ya Juma pili saa 10:24 jioni hadi Jua kuchwa, tutakuwa miongoni mwa wachache watakao bahatika kushudia tukio la angani ambalo limewastaajabisha watu tangu zama za kale. Katika nchi chache za Afrika ya kati, katika eneo mwembamba linaloanzia Bahari ya Pasifiki, kukatisha Gaboni, Zaire, kaskazini ya Uganda, kaskazini ya Kenya karibu na Ziwa la Turkana, Ethiopia na kuishia Somalia, watu wa maeneo hayo watabahatika zaidi kushuhudia Jua likifunikwa kabisa, na kwao mchana utageuka usiku. Kwa upande wetu, nchini Tanzania, tutaona takribani asilimia 70 % ya Jua kufunikwa na kuonyesha Jua likiwa na umbo la hilali kama vile Mwezi mwandamo, linapoangaliwa kwa miwani maaalum ya kuangalizia Jua.

Kupatwa kwa Jua kwa tarehe 3 novemba ni aina maalumu ya kupatwa huko, kunakojulikana kama kupatwa mchanganyiko (Hybrid Eclipse) kwa sababu huanza kama kupatwa kwa pete (Annular Eclipse), ambapo ukingo wa Jua unakuwa haujafunikwa na hivyo kuonekana kama pete. Baada ya muda pete hiyo nayo inafunikwa na kubadilika kuwa kupatwa kamili. Kupatwa kwingine kwa mchanganyiko kuma ule wa Novembar 3 kutatokea tarehe 20 Aprili 2023, katika maeneo ya Asia ya kusini mashariki.

Sisi nchini Tanzania, na takriban bara lote la Afrika (Angalia mchoro wa Afrika), watu wataona kupatwa kwa Jua kwa sehemu asilimia mbali mbali kutegemeana na umbali kutoka mkanda wa kupatwa kamilifu. Hili tukio kubwa kwa vile watu wa bara lote la Afrika watashuhudia tukio hlili kwa pamoja, muda ule ule. Kwa hiyo wananchi barani kote Africa wanahamasishwa wangalie tukio hili la maumbili ya kustajabisha na ni maajabu kwa watoto na vijana kuwachocheza wapende sayansi.

Je kupatwa kunatokeaje? Wakati wa kupatwa kwa Jua, uso wa Jua tunaouona sisi hufunikwaa na Mwezi. Wakati huo, Mwezi unakuwa kati ya Dunia na na Jua, kwa hiyo kivuli cha Mwezi huangukia Duniani. Kutoka angani ungeona kivuli cha Mwezi kinaangukia Dunini (Angalia mchoro wa jiometri unaononesha mistari ya mionzi inayosababisha kivuli.)

Wakati wa kupatwa kwa Mwezi (ambalo lilitokea wiki mbili zilizopita, tarehe 19 Oktoba), pia kuna kufunikwa kwa Jua. Lakini wakati huo Dunia inakua kati ya Jua na Mwazi. Hivyo kivuli cha Dunia kinaangukia Mwezini na kusababisha kiza katika sura ya Mwezi.

Mwezi huzunguka Dunia kila mwezi. Kwa hiyo Mwezi waweza kujipanga mstari mmoja na Dunia na Jua kwa namna ambayo Mwezi uko kati ya Jua na Dunia, na kusababishwa kupatwa kwa Jua. Nyakati nyingine Mwezi unaweza kujipanga mstari kwa namna ambayo Dunia ipo kati ya Jua na Mwezi na kusababisha kupatwa kwa Mwezi.

Kwa vile Mwezi unazunguka Dunia kila mwezi, tungetarajia kutokee kupatwa kwa Mwezi mara moja kwa mwezi, na kupatwa kwa Jua pia mara moja kwa mwezi, yaani tungeshuhudia matukio ya kupatwa mara mbili kila mwezi. Lakini tunaelewa kuwa katika mwaka mmoja, hali ya kupatwa hutokea tatu au nne tu kila mwaka. Kuna tatizo gani?

Dunia inazunguka Jua, na Mwezi unaizunguka Dunia. Na mizunguko hiyo ni ya uso bapa ambayo imeinamia kiasi kidogo. Hivyo, mstari wa Jua, Mwezi na Dunia hauwi wa kunyooka, kupatwa hakuwezi kutokea. Kupatwa kunatokea tu wakati Mwezi unapokuwa pale ambapo mizunguko ya Dunia na Mwezi inakatisha. Hii hutokea mara tatu au nne tu kila mwaka na matokeo ni kwamba tunapata matukio mawili hadi manne tu ya kupatwa kila mwaka.

Sababu nyingine ya Jua kuweza kupatwa na Mwezi ni kwamba unapangalia kutoka Duniani, ukubwa wa Jua na Mwezi zinaukubwa uliolingana kabisa. Ukiangalia Jua kwa kutumia miwani maalumu ya kujikinga, utatambua kuwa Jua linaonekana ukubwa sawa kabisa na Mwezi mpevu. Ingawa kipenyo cha Mwezi ni ndogo, (km3,500), na kile cha Jua ni kikubwa kwa mara mia nne (km. milioni 1.4), vinaonekana ukubwa sawa, kwetu kwa sababu Jua liko umbali wa mara 400 kutoka kwetu. Kwa hiyo ukubwa wao dhahiri ni sawa kabisa. Jambo hili la ulingano kamili wa Jua na Mwezi kutoka hapa Duniani kwetu, ni wa kustaajabisha sana na kinavutia wananchi wote.

Ni rahisi kuonyesha kwa vitendo, kwamba kitu kidogo sana kinaweza kufunika kuona kwako kitu kikubwa sana. Kata mduara mdogo kwenye kadibodi na shika mbali kidogo na macho yako. Utaona kwamba mduara mdgogo unaweza kuficha hata jengo zima au mti wote, jinsi ilivyooneshwa kwenye mchoro.

Pia inavutia kuelewa kwa nini kupatwa kwa Jua hutokea wakati wa Mwezi mwandamo tu. Wakati huo, Jua linakuwa nyuma ya Mwezi, ambao upande wake wa giza unatuelekea sisi. Wakati wa kupatwa kwa Jua, upande mweusi wa Mwezi (upande wenye giza) unakuja mbele ya Jua na kulificha Jua tusilione. Kwa upande mwingine, kupatwa kwa Mwezi, hutokea wakati wa Mwezi mpevu kama ilivyotokea wakati wa kupatwa kwa Mwezi kwa giza jepesi (Penumbral Lunar Eclipse), usiku wa tarehe 19 oktoba 2013. Wakati wa Mwezi mpevu, uso wa Mwezi unaangazwa na Jua kwa ukamilifu na pia linalotuangaza, Duniani upande wa mchana. Fikiria Dunia (yaani sisi) kuwa kati ya Jua na Mwezi. Utaona kuwa kivuli cha Dunia kinaweza kuangukia kwenye Mwezi na kusababisha kupatwa kwa Mwezi. Aina mbili hizo za kupatwa, mara nyingi, hufuatana moja baada ya nyingine, jinsi ilivyotokea safari hii. Mwezi ulipatwa tarehe Oktoba 19 na Jua litapatwa wiki mbili baadaye, yaani tarehe 3, Novemba.

Tumetaja aina mbalimbali za kupatwa kwa Jua: kupatwa kabisa, kupatwa sehemu, kupatwa kwa petu na kupatwa mchanganyiko wa Jua. Kupatwa huku, kunatokea kutegemea na aina ya kivuli cha Mwezi kinachofikia Dunia.

Kama ni kivuli cha giza zito (lijulikanalo kama umbra), hutokea kupatwa kabisa na mwanga wote wa Jua huzibwa. Kusema kweli huu ni miongoni mwa mwonekano wa kustaajabisha katika maumbile kwa sababu mchana ghafla hugeuka kuwa usiku, angalau kwa mda mfupi. Huu ni wakati pekee ambapo mtu anaweza kuona anga la juu la Jua, linalojulikana kamaCorona, ambalo ni muonekano unaofaa kuona mwenyewe. Wanasanyansi wengi wanatumia fursa ya kupatwa kabisa kwa Jua, kufanya utafiti wa Jua na Corona yake na jinis inavyosababisha mabadiliko katika hali ya hewa ya Dunia.

Kupatwa kwa Pete, hutokea wakati kivuli mchanganyiko cha Mwezi kinafikia uso wa Dunia. Kinachotokea hasa ni kwamba Mwezi unakuwa mbali zaidi kutoka Duniani, kwa kipenyo chake dhahiri, ni kidogo kuliko kile cha kipenyo dhahiri cha Jua kwa hiyo ukingo wa Jua unaachwa wazi na pete ya mwanga wa Jua inaonekana.

Tarehe 1 Septemba 2016, Tanzania itakuwa kitovu cha tukio la Dunia wakati kupatwa kwa Jua kwa pete kutapitia Afrika ya kati na kitovu chake kitakuwa kusini mwa Tanzania. Litakuwa ni tukio kubwa kwa Watanzania wote, na kila mtu nchini tujiandae kuwapokea watalii Watanzania pamoja na kutoka nchi za nje kuja kushuhudia tukio hili.

Kupatwa tutakaoona siku ya Jumapili Novemba 3, itakuwa ni kupatwa sehemu tu ya Jua. Sehemu ya Jua itafunikwa na Mwezi. Hakikisha kuwa una miwani maalum ya kuangalizia kupatwa. Aidha, unaweza kutumia kioo Namba 14 kinachotumiwa na wanaochomea chuma. Kwa usalama kamilifu, njia bora zaidi ni kutoliangalia Jua moja kwa moja kwa muda mrefu. Jua ni gimba lina lotoa mwanga mkali mno kupita kiasi.

TAFADHALI USIANGALIE JUA MOJA KWA MOJA, AU KWA DARUBINI - UTAPOFUKA PAPO HAPO.

Kuanzia saa 10:24 jioni, kwa kutumia njia salama ya kuangalia kupatwa kwa Jua, utaona uKingo wa Jua ukianza kufunikwa na Mwezi. Hali hii itadumu pole pole mpaka saa 11:28 jioni wakati kiasi kikubwa cha Jua kitafunikwa. Kwa sehemu za kaskazini ya Tanzania, zaidi ya asilimia 80% ya Jua itafunikwa na mnamo saa 10 jioni wakati watu wa kusini mwa Tanzania wataona asilimia 60% la Jua litakuwa limefunikwa. Jijini Dar es salaam, tunatarajia zaidi ya theluthi mbili za Jua litafunikwa mnamo saa 11 na nusu jioni. Wakati huo, kwa kutumia miwani maalumu, Jua litaonekana kama vile ni Mwezi mwandamo.

Baada ya kupatwa kwa kiwango cha juu, ukubwa wa Jua kama Mwezi mwandamo utaongezeka hadi ukingo wa mwisho wa giza utakapotanzuka saa za magharibi. Mabadiliko ya Jua yatatokea pole pole kwa kipindi cha zaidi ya saa 3 kwa hiyo hakuna haja ya kuangalia kupatwa huko mfululizo na waweza kushirikiana kwa urahisi miwani ya kupatwa kati ya watu wengi.

Licha ya kutumia miwani ya kupatwa na kioo cha giza namba 14, unaweza kuangalia jini kupata kunaendelea kupatwa kwa Jua kwa kutumia njia ya mwonekano. Utakuwa umegundua kuwa mwanga wa Jua unapo ingia kwenye kitundu kidogo chochote kwa mfano katika kipande kikubwa cha kadibodi, utaona mduara wa mwanga ukiangazwa upande wa ndani katika kivuli cha kadibodi. Mduara huo ni taswira ya Jua, na njia hii inaitwa njia ya tundu ya kuangalia kupatwa kwa Jua. Kwa hiyo wakati Jua linapopatwa sehemu tu, utaona umbo kama Mwezi mwandamo badala ya mduara. Utaweza kufatilia kwa urahisi maendeleo ya kupatwa kwa Jua kwa kutumia njia ya mwonekano. Hata mwanga unaopenya kwenye minyare ya kati ya majani ya miti utaonesha Miezi miandamo mingi sakafuni.

Jiandae kwa fursa hii ya kipekee ya kuona tukio la kusisimua Jumapili hii. Kwa maelezo zaidi na taarifa za hivi karibuni, tembelea tovuti: http://www.astronomyintanzania.or.tz

HAKIKISHA KWAMBA UNAKINGA MACHO YAKO KWA MIWANI MAALUM UNAPOANGALIA KUPATWA KWA JUA SIKU YA JUMAPILI 03/09/2013 KWA JUA SIKU YA JUMA PILI 03 NOV, 2013