Semi ni mafungu ya maneno yanayotumiwa kuleta maana nyingine badala ya maana halisi ya maneno yaliyotumika.
Kwa mfano tukisema mtu amegonga mwamba hatumaanishi kwamba amepiga jiwe kubwa kwa mkono au kwa kifaa chochote, bali tunamaanisha kwamba ameshindwa kuendelea katika jambo fulani.
Semi ni kipera cha tungo fupi katika fasihi simulizi; na hutumiwa katika aina nyingine za sanaa kama tamathali za lugha. Kuna fani mbili za Semi: