Ngomezi ni sanaa ya ngoma. Midundo tofauti tofauti ya ngoma hutumika kuwakilisha ujumbe au maana fulani. Ngoma zilitumika sana kabla ya teknolojia ya barua na simu. Wataalam wa ngoma walipiga ngoma kwa milio mbalimbali kufahamisha jamii kwa jambo fulani limefanyika kwa mfano kuingia kwa adui, moto, mtoto anapozaliwa n.k