Wezesha vijana kujiamini, kujiendeleza kiteknolojia, kiufundi, kikazi na kiujasiriamali kupitia warsha za likizo!
Umuhimu wa mitaala ya elimu ya Tanzania inayojikita katika ujuzi msingi ni kuimarisha utoaji wa elimu na mafunzo ili taifa liweze kuzalisha wahitimu wenye uwezo wa msingi katika mawasiliano, ushirikiano, ubunifu, fikra binafsi, kutatua matatizo, ujuzi wa kidijitali, na maadili. Ujuzi huu wote unalingana na mahitaji ya karne ya 21. Ukizingatia ujuzi huo, mafunzo yatakayo zingatia hivi yatawawezesha wahitimu kuwa na uwezo wa kushindana kitaifa, kikanda, na kimataifa na hivyo kukidhi mabadiliko ya kisayansi, kiteknolojia na kiuchumi duniani.
Fungua uwezo wa mtoto wako na warsha za likizo za kujifunza zinazotegemea ujuzi wa AfrikaLearns, zinazopewa nguvu na ujifunzaji kwa kushirikiana na wenzao. Kwa kujiandikisha mtoto wako kwenye warsha zetu, unawapa fursa ya kipekee ya kuendeleza ujuzi muhimu wa karne ya 21 kama vile mawasiliano, ushirikiano, fikira za kina, kutatua matatizo, na ujuzi wa kidijitali. Njia yetu inawawezesha wanafunzi kujifunza kutoka kwa wenzao, kukuza mazingira ya kujifunza yanayochochea ushirikiano wa kweli na wa kuvutia ambao unalingana na ushirikiano wa dunia halisi. Warsha hizi sio tu ziada ya elimu ya jadi bali pia zinawajengea mtoto wako uwezo wa kukabiliana na changamoto za mazingira ya kimataifa yanayobadilika kwa kasi. Wekeza katika mustakabali wa mtoto wako leo kwa kumpa faida ya ujifunzaji wenye msingi wa ujuzi kupitia AfrikaLearns.
AfrikaLearns inaendeshwa na Idara ya Sayansi-Kwa-Vitendo au Science-In-To-Use ya shule ya Africacademy-Arusha Science.
"Napendelea sana mambo ya anga, ndege na urubani. Warsha hizi zimenipa ujuzi wa undani zaidi kuhusu kazi hizi na stadi zinazo takiwa ili kufanikiwa".
Jaqueline Kanuya
"Kumbe kutengeneza roboti ni kitu rahisi hivi!"
Sandra Bhurian
"Sikuwa na uwezo wa kuongea mbele za watu. Baada ya mazoezi mazuri kupitia AfrikaLearns, nataka niendeshe mikutano ya wanafunzi wenzangu na kuzungumza nao mweyewe bila hofu".
Khalid Kanka
"Kuongea na vijana wa chuo wanao jielewa kimenisaidia kuona mimi pia ninaweza".
Adam Majura
Jenga umahiri kupitia warsha za likizo fupi na ndefu
Kutanishwa na vijana wenye shauku na stadi
Gharama nafuu za warsha zenye thamani kubwa
"Kujifunza kutoka kwa wenzangu ni bora zaidi. Tuna elewana sana kwasababu tunalingana".
Dorcas Maudi
"Kama mwanafunzi wa la saba nimepata ujuzi zaidi ya wenzangu darasani. Naweza kuwafundisha vitu vipya kwasababu nimepata fursa hii. Nangojeaga likizo kwa hamu sana maana najua nitakuwa naboresha ninacho soma shuleni kwa undani zaidi".
Grace Mawilitisa
"Sikujua baadhi ya kazi na fursa zilizopo nchini na nje ya nchi za kombi zangu za masomo. Kuna vitu vingi wanafunzi hawajui lakini ndani ya siku moja nime jua fursa kama 10 mpya kabisa!"
Koko Georgies
"Kujifunza kuhusu teknologia mbalimbali ambazo hata hapa nchini hazitumiki, ni kitu kinacho tufungua macho na fikra juu ya uwezo wetu kwenye kuvitengeneza au kuvitumia".
Elizabeth Cuthbert
👇🏾JAZA FOMU KUSHIKA NAFASI SASA!👇🏾